Nyuki-kekeo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyuki-kekeo
Coelioxys froggatti
Coelioxys froggatti
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno kipana)
Familia ya juu: Apoidea
Latreille, 1802
Ngazi za chini

Familia 3 zenye nyuki-kekeo na jenasi 8 katika Afrika ya Mashariki:

Nyuki-kekeo (kutoka kwa Kiing. cuckoo bees) ni nyuki waliotaga mayai yao katika viota vya nyuki wengine, kama vile kekeo hufanyia ndege wengine. Kuna makundi mbalimbali ya nyuki-kekeo. Jenasi iliyoenea zaidi na kuwa na spishi nyingi barani Afrika ni Coelioxys ya familia Megachilidae yenye spishi 21 katika Afrika ya Mashariki. Jenasi nyingine ya familia hii, Euaspis, ina spishi chache, ambazo moja tu imerekodiwa kutoka Afrika ya Mashariki. Makundi mengine hutokea katika familia Apidae, muhimu zaidi duniani kote ikiwa nusufamilia Nomadinae yenye spishi 14 katika Afrika ya Mashariki. Kabila Melectini ina spishi 20 za Afrika ya Mashariki katika jenasi Afromelecta na Thyreus. Makabila mengine nne zilizo na nyuki-kekeo hazipatikani Afrika (Bombini, Ericrocidini, Euglossini na Isepeolini). Katika familia Halictidae jenasi Sphecodes ina spishi 6 za nyuki-kekeo katika Afrika ya Mashariki.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Kwa sababu nyuki hawa wako katika makundi mbalimbali ya kitaksonomia, haiwezekani kutoa maelezo ya wao wote pamoja. Tembelea kurasa maalum kwa taarifa zaidi. Hata hivyo, kwa ujumla, nyuki hawa hawachomi au mchomo wao sio chungu hasa. Pia huwa na kutikulo ngumu kuhimili mashambulizi ya mdusiwa wao. Kwa sababu hiyo hiyo, wanaweza kuwa na marekebisho mengine.

Kama jina lao linavyoonyesha, nyuki hawa wana tabia kama kekeo kwa maana kwamba wao pia hawajengi viota vyao wenyewe, lakini hutaga mayai kwenye viota vya nyuki wengine, kwa kawaida wapweke. Nyuki mdusiwa wanaweza hata kuwa katika kundi moja la kitaksonomia na wanaweza kuwa na uhusiano wa karibu. Spishi nyingine hudusia nyuki wasiohusiana, pengine spishi mdusiwa moja tu au vinginevyo spishi kadhaa.

Spishi za Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]

Apidae

Apinae
  • Afromelecta bicuspis
  • Afromelecta lieftincki
  • Thyreus abyssinicus
  • Thyreus albomaculatus
  • Thyreus axillaris
  • Thyreus bouyssoui
  • Thyreus calceatus
  • Thyreus delumbatus
  • Thyreus forchhammeri
  • Thyreus interruptus
  • Thyreus kilimandjaricus
  • Thyreus meripes
  • Thyreus neavei
  • Thyreus niloticus
  • Thyreus pictus
  • Thyreus pretextus
  • Thyreus scotaspis
  • Thyreus splendidulus
  • Thyreus tschofferi
  • Thyreus vachali
Nomadinae
  • Epeolus amabilis
  • Epeolus corniculatus
  • Epeolus natalensis
  • Pasites barkeri
  • Pasites carniflex
  • Pasites friesei
  • Pasites humecta
  • Pasites jonesi
  • Pasites rotundiceps
  • Schwarzia emmae
  • Schwarzia elizabethae
  • Schwarzia gretae
  • Schwarzia icipensis
  • Schwarzia lualenyiensis

Halictidae

  • Sphecodes fulleborni
  • Sphecodes hagensi
  • Sphecodes luteiventris
  • Sphecodes nyassanus
  • Sphecodes quadrimaculatus
  • Sphecodes ugandae

Megachilidae

  • Coelioxys albomarginata
  • Coelioxys ateneata
  • Coelioxys caeruleipennis
  • Coelioxys caffra
  • Coelioxys capensis
  • Coelioxys cherenensis
  • Coelioxys cyanura
  • Coelioxys haemorrhoa
  • Coelioxys loricula
  • Coelioxys maculata
  • Coelioxys nasuta
  • Coelioxys natalensis
  • Coelioxys odin
  • Coelioxys recusata
  • Coelioxys scioensis
  • Coelioxys selosa
  • Coelioxys squamatula
  • Coelioxys torrida
  • Coelioxys ultima
  • Coelioxys umbripennis
  • Coelioxys verticalis
  • Euaspis abdominalis

Picha[hariri | hariri chanzo]