Nyankende
Nyankende ni kata ya Wilaya ya Kahama Vijijini katika Mkoa wa Shinyanga, Tanzania. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 14,515 waishio humo.
Kata ya Nyankende ilifanikiwa kuwa na zahanati mwaka 2014 ambapo ilijengwa katika kijiji cha Nyankende pia ilipofika mwaka 2015 iliweza kupata shule moja ya sekondari iliyopewa jina la Nyankende huku wakianza na walimu saba tu ikiwemo wawili wa sayansi na watano masomo ya sanaa mbali na hilo ina shule za msingi sita: 1. Nyankende 2. Bunanda 3. Sinwankere 4. Kagera 5. Akzyoba na 6. Nyambeshi.
Pia kijiji cha Bunanda baadae 2016 kilianzishiwa zahanati ya pili kuleta jumla ya zahanati 2 katika kata ya Nyankende.
Kwa kumalizia kuna miradi mikuu miwili: wa kwanza ni maji na wa pili umeme ambao bado utekelezaji haujaanza [1]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
![]() |
Kata za Wilaya ya Kahama Vijijini - Mkoa wa Shinyanga - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Bugarama | Bukomela | Bulige | Bulungwa | Bulyanhulu | Busangi | Chambo | Chela | Chona | Idahina | Igunda | Igwamanoni | Isaka | Jana | Kashishi | Kinamapula | Kisuke | Lunguya | Mapamba | Mega | Mpunze | Mwalugulu | Mwanase | Ngaya | Ntobo | Nyankende | Sabasabini | Segese | Shilela | Ubagwe | Ukune | Ulewe | Ulowa | Ushetu | Uyogo |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Shinyanga bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Nyankende kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |