Muhammed Said Abdulla

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Muhammed Said Abdulla (25 Aprili 1918 - Machi 1991) alikuwa mwandishi kutoka kisiwa cha Unguja katika nchi ya Tanzania. Anasifiwa kuwa mwandishi wa kwanza aliyefaulu kupata wasomaji wengi kwa riwaya zake zilizoandikwa kwa Kiswahili. [1]

Maisha yake

Muhammed Said Abdulla alizaliwa huko Makunduchi kisiwani Unguja. Elimu yake ya sekondari aliipata katika shule ya misheni ya Kikristo. Baada ya kumaliza masomo mwaka 1938 aliajiriwa na serikali kwenye idara ya afya. Halafu alihamishiwa idara ya kilimo alipokuwa mhariri wa jarida la Swahili Bulletin. [2].

Kutoka hapo aliendelea kuwa mwandishi wa habari na kuanzia 1948 akawa mhariri wa gazeti la Zanzibari. Baadaye alikuwa mhariri msaidizi wa majarida ya Al-Falaq, Afrika Kwetu na Al Mahda. Tangu 1958 hadi kustaafu mwaka 1968 alikuwa mhariri wa jarida la Mkulima. Katika kipindi hiki kilitokea mapinduzi ya Zanzibar ambako mke na watoto wake waliuawa.

Riwaya

Mwaka 1958 Abdulla alishiriki kwenye mashindano ya utunzi wa tungo za Kiswahili ("Swahili Story-Writing Competition") yaliyoendeshwa na Ofisi ya Fasihi ya Afrika ya Mashariki (East African Literature Bureau). [3] Riwaya yake Mzimu wa Watu wa Kale ilishinda tuzo la kwanza ikachapishwa kitabu 1960. Hapa alimbuni mhusika Bwana Msa aliye mpelelezi wa binafsi anayeshirikiana na polisi na kudhihirisha siri ya uuaji wa mtu tajiri. jina la "msa" ni akronimi ya herufi za kwanza za majina yake mwenyewe Abdulla yaani M-S-A.

Abdulla aliendelea kutunga kwa jumla riwaya ya upelelezi sita ambako Bwana Msa ni mhusika mkuu. Mhusika huyu anafanana katika tabia kadhaa na Sherlock Holmes, mhusika wa riwaya za mwandishi Mwingereza Conan Doyle. Sawa na Sherlock Holmes Bwana Msa anavuta kiko, anapata usulihisho wa kesi kwa kutumia akili yake akishirikiana na msaidizi na rafiki yake Najum (anayefanana na Dr. Watson wa Sherlock Holmes) na kusaidia kazi ya polisi inayowakilihswa na Spekta Seif.

Wahakiki walimshambulia Abdulla kwa kutumia mfano wa kigeni.[4] Hata hivyo hata akitumia nukuu za Conan Doyle aliweka masimulizi kabisa katika mazingira na utamaduni wa Unguja na jamii ya Waarabu na Waafrika kabla ya mapinduzi.

Wahakiki wengine wameona ya kwamba muundo wa kesi katika hadithi za Abdalla ni tata mno, hata hivyo wamemsifu kwa uwezo wake wa kuchora tabia za wahusika kikamilifu katika lugha na imani ya Kiunguja.[5]

Kati ya riwaya zake za kipelelezi ni:

Nje ya riwaya za upelelezi aliandika pia Mke Mmoja Waume Watatu (1975) kinachohusu ulaghai katika ndoa na mkusanyo wa hadithi fupi katika "Hekaya za Kuburudisha".

Wasifu

Abdulla alikuwa ni mhariri na mwaandishi wa vitabu tofauti ambavyo viliinyanyua lugha ya kiswahili katika daraja la juu na kuiongezea umaarufu mkubwa eneo la afrika mashariki. Alifanikiwa kuowa mke na kupata wawili katika maisha yake. Vile vile ni miongoni mwa watetezi wakubwa walifanya utetezi katika kuikomboa nchi ya Zanzibar kutoka mikononi mwa Watanganyika. Na hii ndio ilikuwa sababu ya yeye kuwa katika hatari ya maisha yake. Miongoni mwa beti zake za kuwatupia watanganyika ujumbe utakaoweza kuwapotezea nguvu ya kutaka kuinyakuwa Zanzibar. Njama ilianza kupangwa na watanganyika ili kumuondoa Bwana Msa Katika hii dunia. Aliuwawa yeye na familia yake, mkewe na watoto wake wawili wa kike katika kipindi cha mapinduzi ya Zanzibar. Hili lilikuwa pigo kubwa sana kwa Wazanzibari wote kwa kuuwawa Bwana Msa katika mazingira ya kutatanisha.

Tanbihi

  1. https://www.britannica.com/biography/Muhammed-Said-Abdulla
  2. Zúbková, Elena Bertoncini (2008). "Abdulla, Muhammed Said". In Akyeampong, Emmanuel K.; Gates, Henry Louis Jr. Dictionary of African Biography. Oxford University Press. ISBN 978-0-19-538207-5; iliangaliwa Machi 2017 kupitia google-books
  3. Wakati ule waandishi wengi Waafrika waliingia katika mashindano haya, 1956 ni Shaaban Robert aliyeshinda tuzo.
  4. Kamau uk.16
  5. linganisha makala ya Zúbková

Marejeo

Makala hii kuhusu mwandishi fulani wa Afrika bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Muhammed Said Abdulla kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.