Mtumiaji:Kipala/Archive 13

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ukurasa mama: Majadiliano ya mtumiaji:Kipala

Huu ni ukurasa wa nyaraka kwa miaka 2019


Kupinga makala kufutwa ya Mr Puaz

Hello Kipala, nimeona UJUMBE was kufutwa kwa makala ya Mr Puaz na ningependa uipitie Tena maana Sasa Ina vyanzo vinavyoonyesha utambulisho was Sanaa ya my huyo.

Asante. Ndizibanana (majadiliano) 09:33, 21 Januari 2019 (UTC)

Omnivore

Kipala salaam. Kwa kuwa sasa tumekubali kwamba hatupendi mlawangi, tutatumia istilahi gani? Tufuate KBFK na kutumia mlavyote? ChriKo (majadiliano) 06:31, 30 Januari 2019 (UTC)

Document your culture with Wiki Loves Love 2019 and win exciting prizes!

Please help translate to your language

Africa has many beautiful festivals, ceremonies and celebrations of love and we need your help to document these! They are the core part of African culture and in order to make sure this way of life followed by our ancestors remain among us, we need to have them online to make sure they are preserved. Join hands with Wiki Loves Love that aims to document and spread how love is expressed in all cultures via different rituals, celebrations and festivals and have a chance to win exciting prizes!! While uploading, please add your country code in the Wikimedia Commons upload wizard. If you want to organize an on-site Wiki Loves Love event, then contact our international team! For more information, check out our project page on Wikimedia Commons.

There are several prizes to grab. Hope to see you spreading love this February with Wiki Loves Love!

Imagine...The sum of all love!

Wiki Loves Love team 07:34, 4 Februari 2019 (UTC)

Rafu ya bara

Ndugu, nimejibu swali lako kuhusu tako la bahari, ila sijaona itikio lolote. Kumbe umebadilisha kazi yangu kuhusu visiwa. Kwa nini kupunguza viungo vya jamii ambavyo vinaweza kuvutia watu kusoma kurasa zetu? Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:59, 10 Februari 2019 (UTC)

Asante, mchango wako kuhusu tako la bahari naona sasa tu maana ulichangia mahali ambako sikutegemea. Kuhusu visiwa nilianza lakini sasa nasita kwa kwa sababu nilitambua sikutafakari vema labda tushauriane tena (na toba yangu kurudia kila kitu..). tatizo ninaloona tukiwa na vitu vingi katika jamii moja hatuna budi kuvipnga kwa vikundi vidogo. Kwa hiyo ni nilianza jamii:Visiwa vya Ziwa Viktoria (inayounganishwa katika Jamii:Ziwa Viktoria na pia Jamii:Visiwa vya Tanzania) nikaona naweza kufuta mengine. Mpaka kuona ya kwamba tukiendelea na visiwa vya ziwa tutapata pia visiwa vya Kenya na Uganda, kumbe sikufikiri adi mwisho. Subiri, nirudi nyumbani (niko kwenye kikao cha kuchosha) na kutafakari upya.Kipala (majadiliano) 12:50, 10 Februari 2019 (UTC)
Mzee, tuko pamoja. Ni kweli kuna jamii zenye viungo vingi mno, na mimi nimechangia sana hali hiyo katika kuunganisha mito ya Tanzania na Bahari ya Kati moja kwa moja! Samahani kwa hilo. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:07, 10 Februari 2019 (UTC)

Bibi Titi Mohamed

Sijui kwa nini umefuta masahihisho yangu... --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:42, 6 Aprili 2019 (UTC)

RE:Mgeni Kutoka Ughaibuni

Salaam! Makala ya kufuta ile. Haielezi kama ni riwaya au kitu gani. Sioni chochote ndani yake! Wasalaam!--Muddyb Mwanaharakati Longa 07:56, 15 Aprili 2019 (UTC)

Naomba fanya wewe. Wewe mtaalamu wetu kuhusu fasihi ya Kiswahili. Kipala (majadiliano) 08:43, 15 Aprili 2019 (UTC)

Wingi wa dawa

Kipala salaam. Ninachanganyikiwa kuhusu wingi wa neno "dawa". Ninaona "dawa za" na "madawa ya". Ninapata wazo la kwamba ile ya kwanza hutumika kwa dawa za kutibu na kuua viumbe visumbufu, na ile ya pili kwa madawa ya kulevya. Hii ni sahihi? ChriKo (majadiliano) 13:43, 13 Mei 2019

Nadhani hakuna tofauti ya maana. Dawa kisarufi iko pande zote mbili. KKS: Dawa nm [i/zi] pia ma [li/ya]. Vivyo hivyo kamusi za zamani. Fanya tu jinsi unavyopenda. Kipala (majadiliano) 14:51, 13 Mei 2019 (UTC)
Asante sana. ChriKo (majadiliano) 19:48, 13 Mei 2019 (UTC)

Rutongo

Hi, dearest Kipala, how are you? Me fine!!!

Please, I've opened this page, that remembers me a class-mate from this city. Can you put some news more in the story of the city, please? I'll be pleased to help you in Italian and Portuguese. Thanks a lot for your help!!!

Rei Momo (majadiliano) 09:30, 2 Juni 2019 (UTC)

Wanafunzi?

Ndugu, kuna watu wanafanya warsha ya kuandika kwenye Wikipedia? Naona kuna makala nikadhani labda ni wanafunzi wanajarijaribu hivi. --Ndesanjo (majadiliano) 13:03, 9 Juni 2019 (UTC)

Ndiyo, ni wanafunzi wa Alfagems Morogoro. Niko nao. Wengine wameshapiga hatua, wengine bado. Ndio kesho ya Wikipedia yetu. Wakikosea, narekebisha. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:06, 9 Juni 2019 (UTC)
Ni vizuri nimeuliza. Nilishangaa kidogo. Nilifuta moja ya mwanafilamu Kanumba baadaye ninaona makala nyingine na majina mapya zinajitokea. Nikaona si kawaida, ngoja niulize. Hongereni. Ni vizuri sana. Tutawaidia. Wape salamu. Kweli hawa ndio wahahari wa kesho. --Ndesanjo (majadiliano) 13:14, 9 Juni 2019 (UTC)


Utendi

Ndugu, ni kweli KKK inaonyesha utendi na utenzi ni kitu kimoja, lakini sisi wanakanisa tumezoea kutumia neno utenzi kwa maana ya pekee, si utenzi wa shujaa (epic) tu kama utendi, bali hasa wa kiroho. Pia kuhusu koloni, nimeona ulivyosema kuwa toleo la pili la KKS linaweka ngeli i-zi, lakini la tatu linarudi kusema li-ya. Shalom. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:10, 18 Juni 2019 (UTC)

Naona kiasili neno ni lileile ila zaidi swali la lahaja (kama ni d badala ya s/z, naona dalili la Kiamu, kiasili ḏ/dh kutoka ara. ذ). Kutokana hapa tahajia mbili, na unavyosema "utenzi, tenzi" imekuwa kawaida kwa nyimbo za kikristo, lakini sijui kama watu wasio Wakristo wanijua.Basi naongeza mstari, sawa? Kipala (majadiliano) 12:59, 18 Juni 2019 (UTC)

Administrative division of Côte d'Ivoire

Hello Kipala, Can you, please, give your opinion on this question? Thanks in advance. --Zenman [Majadiliano] 18:48, 21 Juni 2019 (UTC)

Re:mail

Hi, you can check randoms user’s edits. The 90% are external links to commercial sites. —Wim b (majadiliano) 10:37, 4 Julai 2019 (UTC)

  1. Last edit: special:diff/1053323
  2. Special:Permalink/1048813
  3. Special:permalink/1022011 link to http://phgardencity.com/phenq-review/ and https://www.webmd.com/diet/news/20000322/drinking-green-tea-may-help-you-lose-weight#1
  4. special:diff/1022006 link to https://www.webmd.com/diet/news/20000322/drinking-green-tea-may-help-you-lose-weight#1 (and 2 times) and http://studentorganisations.uonbi.ac.ke/ccpe/has-anyone-tried-phenq/
  5. special:diff/1020449 (reverted and dead site now)
  6. special:permalink/1010385 3 links to "increasetestosterone" and a to https://www.healthline.com/health/boost-your-libido-10-natural-tips
  7. special:permalink/1016293 link to beanbagsexpert (2 times)
  8. special:permalink/1016295 2 links
  9. special:permalink/1016717 link to https://wikitravel.org/en/Las_Vegas and another
  10. special:diff/1016275
10 exemples of spam in half first edit's page. --Wim b (majadiliano) 18:57, 4 Julai 2019 (UTC)
ok,lots of bullshit. From the numbers (and his edits at swwiki) I see he has been editing with little quality but has not tried to push any specific sites. No mass spamming, no obvious malicious editing. Over there at global oversight do you have a policy not to try talking to and educating people? I just wonder when I see one arm of Wikimedia tries to improve "literacy" for African internet public (lamenting "white spots on the map of knowledge" in Africa) and on the other side I see that contributions from here get thrown out and people blocked all the time without ever been guided how to improve. Looks a bit biblical "do not let your left hand know what your right hand is doing” (Matthew 6:3). Or? Kipala (majadiliano) 20:06, 4 Julai 2019 (UTC)
He has not tried to push any specific sites, but many sites. --Wim b (majadiliano) 17:48, 5 Julai 2019 (UTC)
Wim, I have to retract my argumentation for this case. He put into one article links to http://freelancinghackers.com/2017/06/17 and disguised these as literature links. His price for wikipedia links was 30 USD. Ok, white flag from my side. Thanks for giving your time. Kipala (majadiliano) 18:24, 5 Julai 2019 (UTC)
No problem :) --Wim b (majadiliano) 10:33, 6 Julai 2019 (UTC)
I am seriously concerned with your apparent inability to recognize that this user, among others, are spamming links that decrease the quality of this project. The additions are, without a doubt, spam, mostly of illegitimate websites seeking profit. It's also very concerning that you reply to a well-meaning steward by referring to his comments as "lots of bullshit". Your actions are not indicative of a responsible administrator and bureaucrat. Vermont (majadiliano) 18:00, 5 Julai 2019 (UTC)
Vermont, I learned that it is generally fruitful to ask back before shooting from the hip. Try to imagine that the quoted "bullshit" did not refer to what you decided to see, but was about the listed links. Which may be more logical for a clause that starts with an agreeing expression "ok". Kipala (majadiliano) 18:24, 5 Julai 2019 (UTC)
I apologize, I misinterpreted that; thank you for your clarification. What still stands, however, is that you seem to oppose the lock of spambots and the removal of their spam, which is a problem. Vermont (majadiliano) 19:41, 5 Julai 2019 (UTC)
Thanks for civilty. Just: did we discuss a spambot? And perhaps have a look upstairs, I replied to Wim above your first lines, as I answered you separately.Kipala (majadiliano) 19:45, 5 Julai 2019 (UTC)
Yep, thanks for your response above. And no, it seems spambot was a mistype. Meant spammers. Thanks, Vermont (majadiliano) 03:39, 6 Julai 2019 (UTC)

Shule za Tanzania

Vipi mzee? Kwa muda mrefu nilitaka kukuuliza kama inafaa shule ziwe na kurasa katika Wikipedia. Mwanafunzi wetu alipoanzisha mmoja kuhusu Alfagems niliweka alama ya kufuta, lakini sikuufuta. Sasa Innocent Massawe ameanza kutunga kurasa za namna hiyo. Je, aendelee? Pia nimeona michango yako ya mwisho haionekani katika "mabadiliko ya karibuni": imekuwaje? Shalom! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:50, 21 Agosti 2019 (UTC)

Salaam, narudi TZ wiki ijayo. Kuhusu shule naona tusikubali zote isipokuwa kama ni shule za pekee. Hapa tunaweza kutumia swali la ushahidi, nje ya blogu na orodha za intaneti. Kama shule ilikuwa na maana hadi kujadiliwa (si kutajwa tu) katika kitabu au makala za kitaalamu ningeunga mkono. Mfano Tabora Boys, niliyokuta mara nyingi kuwa shule ya wavulana Waafrika wakati wa ukoloni, na viongozi mbalimbali wa uhuru walisomeshwa kule. Kuhusu michango yangu kutoonekana nimeona tatizo pia lkn sijatambua bado imafuata mfumo gani. Kipala (majadiliano) 11:34, 21 Agosti 2019 (UTC)

Templates

Hey, I saw a bunch of issues with templates, especially cite book/journal and this is probably what is causing it. Praxidicae (majadiliano) 18:14, 23 Agosti 2019 (UTC)

I don't undertand what you have said because the templates are mysterious to me!!! Let's inform Kipala or Muddyb. Peace to you. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:08, 24 Agosti 2019 (UTC
It might be helpful if you name the templates you came about. We hve swahilized a number of templates but find the recent ones a bit complicated. Thus have to look for work-arounds. Kipala (majadiliano) 19:40, 27 Agosti 2019 (UTC)

Atomi

KKK inapendelea atomi, ingawa haikatai atomu. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:56, 9 Septemba 2019 (UTC)

Hori

Hori la? Si hori ya? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:57, 19 Septemba 2019 (UTC)

Kweli kabisa, asante! Tusahihishe. Kipala (majadiliano) 15:14, 19 Septemba 2019 (UTC)
Pia kwa Kiingereza kuna shida kati ya ghuba na hori: haieleweki majina hayo yanavyotumika. Kwa nini Kiswahili kifuate fujo ya lugha hiyo badala ya kutofautisha ghuba na hori (ambayo ina mdomo mwembamba)? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:30, 24 Septemba 2019 (UTC)

Mafikirio tu

Natamani kafanya kazi na uongozi huu wa wikipedia (mchango wa mtumiji:Chusaki ya 19:02, 5 Novemba 2019)‎

Karibu sana. Tafadhali uzoee kutia sahihi kwa kumaliza kwa alama za ~~~~. Kipala (majadiliano) 19:50, 5 Novemba 2019 (UTC)

Makala 1,000 za msingi

Ndugu, zimebaki 14 tu: tumekula ng'ombe, kwa nini tusindwe na mkia? Naomba tujitahidi kumalizia hizo, ingawa ni ngumu, halafu tuendelee na zile 10,000. Sijui ulipata wapi baadhi ya maneno, kama uhusianifu majumui. Pia infinity ina alama za ulizo: nilitaka kujaribu "usokomo". Unasemaje? Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:46, 12 Novemba 2019 (UTC)

kwa kweli sehemu ya mada zilizobaki sielewi kabisa wala kwa Kijerumani wala kwa Kiingereza kwa hiyo sikutaka kuanza kwa Kiswahili. Kuhusu chanzo cha maneno uliyotaja , naomba usubiri kidogo niko safari sasa hivi. Mara nyingi kama hamna ktk Tuki, natafuta kwa KAST. Kipala (majadiliano) 09:51, 12 Novemba 2019 (UTC)

Kutaka kubadili jina la mtumiaji wikipedia

Mimi mi mwanafunzi wa Alfagems,naomba kuuliza jinsi ya kubadili jina langu la Wikipedia bila ya makala zangu kufutika yaani niendelee na makala zangu zilizopo bila ya kuanza upya---Simon waziri msika kutoka Alfagems.

Habari Simon, una njia mbili.
1) Njia nyepesi ni KUUNDA AKAUNTI MPYA, wakati ukiacha akaunti ya kwanza jinsi ilivyo na kutoitumia. Hii unaweza kufanya mara moja. a) Kwenye akaunti ya zamani unafungua ukurasa wa mtumiaji, unaweka alama za {{retired}} mwishoni au mwanzoni, hifadhi ukurasa . b) unalogout. c) unaanzisha akaunti mpya. d) kama umetumia watchlist, unaweza kuihamisha kwa maelezo yafuatayo: https://en.wikipedia.org/wiki/Help:Copying_watchlist_to_new_username

2)a) Fungua ukurasa wa https://en.wikipedia.org/wiki/Wikipedia:Changing_username/Simple, usome yote na kubofya sehemu ya "Click here to request a username change"
AU
b)Njia nyingine ni kufungua https://en.wikipedia.org/wiki/Special:GlobalRenameRequest na kuingiza jina unalotaka

Ukitumia njia ya pili mtu atakayefungua makala zako za awali ataona jina la awali halafu akifuata jina lako la awali atapelekwa kwa ukurasa wako mpya. Kipala (majadiliano) 14:41, 24 Novemba 2019 (UTC)

Kuhusu kufutwa kwa Wikipedia ya Denis RJ

Nimetoa mchango wangu lakini ndugu Kipala amefuta sijui kwanini. Ili hari msaanii niliechangia ni msanii halisi kabisa. Kwasasa anawimbo mmoja na ameshautoa, au Wikipedia inawahusu wakina nani., Acha ubaguzi huo Bwana Kipala🙏🙏 Mikuyu Denis (majadiliano) 15:14, 30 Desemba 2019 (UTC)

Mpendwa makala jinsi ulivoiacha haikuonyesha dalili yoyote kama mtu huyu ana umaarufu fulani. Pia ulitangaza (nikikumbuka vema) anwani zake kwenye mitandao ya kijamii. Kwa bahati mbaya tunapata hapa mara kwa mara watu wanaojaribu kujitangaza ambayo haikubaliki, na makala yako ilifanana na hiyo kabisa. Wimbo mmoja haiundi umaarufu bado. Tadadhali usome mwongozo na sehemu ya umaarufu. Karibu sana kuchangia tena kwenye msingi imara.Kipala (majadiliano) 15:54, 30 Desemba 2019 (UTC)