Mpito wa sayari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mpito wa Zuhura mbele ya Jua tar. 21.12.2012

Mpito wa sayari (ing. planetary transit) unamaanisha hali ya sayari kupita kati ya Jua na Dunia na hivyo kufunika sehemu ya Jua. Tofauti haionekani kwa macho lakini inaweza kutazamwa kwa kutumia darubini.

Kuna sayari mbili zinazoweza kupita mbele ya Jua kwa macho ya mtazamaji duniani: Utaridi (Mercury) na Zuhura (Venus).

Nje ya mfumo wa Jua mpito wa sayari-nje isiyoonekana kwa darubini (kutokana na umbali wake) mbele ya nyota inasababisha mabadiliko ya mng’aro wa nyota ile na hayo yanathibitisha kuwepo kwa sayari-nje na pia kukadiria obiti na tabia nyingine.

Tazama pia

Marejeo

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mpito wa sayari kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.