Mohamed Tahar Fergani

Mohamed Tahar Fergani (9 Mei, 1928 - 7 Desemba, 2016) alikuwa mwimbaji wa nchini Algeria, mpiga fidla na mtunzi, aliyepewa jina la utani la Nightingale of Constantine.
Maisha ya awali
[hariri | hariri chanzo]Alizaliwa huko Constantine . Akiwa kama mwalimu wa muziki wa Malouf Constantine. Mohamed Tahar Fergani ni mmoja wa waimbaji wachache kutafsiri utunzi wa oktoba 4. Mbali na Malouf, anafasiri Mahjouz (aina maarufu ya Constantinois inayotokana na Malouf), Zjoul (aina ya muziki wa zamani kama Malouf, Constantinois) na Hawzi (aina maarufu inayotokana na Tlemcen Gharnati).
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Baba yake Hamou Fergani alikuwa mwimbaji wa Hawzi. Mohamed Tahar alianza katika muziki wa mashariki, baadae alibadilisha mtindo na kwenda kwenye Malouf. Mohamed Tahar ana mamia ya rekodi, alipokea tuzo kadhaa za kimataifa. Aliunda Orchestra na shule yake ya Constantine. Moja ya nyimbo zake zinazojulikana nchini Algeria ni kama "Ed Dhalma" , alifariki mjini Paris akiwa na umri wa miaka 88 tarehe 7 Desemba 2016. [1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mohamed Tahar Fergani kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |