Mlimani City

Mlimani City ni duka kubwa lililopo katika barabara ya Sam Nujoma, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, Tanzania.
Ni moja ya maduka makubwa zaidi nchini Tanzania[1], yenye eneo la ukubwa wa mita za mraba m2 30 000 (sq ft 320 000). Sherehe ya ufunguzi ilikuwa Novemba mwaka 2006. Ni duka la kwanza nchini Tanzania lenye viyoyozi.
Mlimani City hupatikana maduka kadhaa ya rejareja, migahawa, na majumba ya sinema[2]. Miongoni mwa maduka hayo ni maduka pendwa ya Afrika Kusini na India kama Choppies ambayo kwa hakika yanapatikana nchini Botswana na kwa Mr. Price.
Ukumbi wa Mikutano
[hariri | hariri chanzo]
Ukumbi wa Mlimani City ni mojawapo ya majengo hapo Mlimani City, ukumbi huu unaweza kuwa mahsusi kwa ajili ya mikutano, harusi, makongamano na sherehe mbalimbali za watu binafsi na kitaifa.[3]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Major Mlimani City expansion project to cost $100 million". The Citizen (kwa Kiingereza). 2021-03-30. Iliwekwa mnamo 2025-09-14.
- ↑ Century Cinemax Tanzania. "Century Cinemax Tanzania | Premium Cinema Experience". Century Cinemax Tanzania (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-09-14.
- ↑ https://www.mlimanicity.co.tz/conference
| Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|