Mfenesi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mfenesi
(Artocarpus heterophyllus)
Mfenesi
Mfenesi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Rosales (Mimea kama mwaridi)
Familia: Moraceae (Mimea iliyo na mnasaba na mforosadi)
Jenasi: Artocarpus
Spishi: A. heterophyllus
Lam.

Mfenesi (jina la kisayansi Artocarpus heterophyllus; kwa Kiingereza Jackfruit, Jack tree n.k.) ni mti wa familia Moraceae.

Tunda lake huitwa fenesi na ni tunda la mti lililo kubwa kabisa kuliko matunda ya mti yote (hadi kg 36 na sm 90x20). Hata hivyo, mti mmoja unaweza kuzaa matunda 100 hadi 200 kwa mwaka.

Mbao za mti huo ni nzuri kwa utengenezaji wa fenicha mbalimbali.

Asili ya mti huu ni Uhindi. Siku hizi hupandwa mahali pengi pa kanda ya tropiki ambapo kunanyesha kiasi.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mfenesi kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.