Maghrib

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nchi za Maghrib leo

Maghrib (المغرب العربي al-maġrib al-ʿarabī; pia: Maghreb) ni sehemu ya kaskazini-magharibi ya Afrika.

Siku hizi jina linataja nchi za Moroko, Algeria na Tunisia, wakati mwingine pia Mauretania na Sahara Magharibi.

Zamani lilimaanisha tu maeneo kati ya pwani ya Bahari Mediteranea na vilele vya Milima ya Atlas pamoja na sehemu za Rasi ya Iberia (Hispania kusini na Ureno), Malta na Sisilia zilizotawaliwa na Waislamu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Maghrib kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.