Rasi ya Iberia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rasi ya Iberia jinsi inavyoonekana kutoka anga ya nje

Rasi ya Iberia ni kati ya rasi kubwa za Ulaya ikiwa na eneo la km² 582,860. Iko kusini magharibi mwa Ulaya ikipakana na Bahari Atlantiki upande wa kaskazini na magharibi, halafu Bahari Mediteranea upande wa kusini na mashariki.

Milima ya Pirenei ni mpaka kati ya rasi na Ufaransa (Ulaya ya magharibi).

Iberia ni jina la kale tangu zamani za Waroma wa Kale.

Nchi na maeneo[hariri | hariri chanzo]

Kwenye rasi kuna nchi zifuatazo:

  • Hispania ni nchi kubwa kwenye rasi
  • Ureno iko upande wa magharibi
  • Andorra ni nchi ndogo sana katika milima ya Pirenei kati ya Hispania na Ufaransa
  • Gibraltar ni eneo ndogo la Uingereza katika ncha ya kusini inayotazamana na Afrika.
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Rasi ya Iberia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.