Nenda kwa yaliyomo

Liturujia ya Kimungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mozaiki ya mwaka 1150 hivi inayoonyesha watakatifu Basili Mkuu (kushoto) na Yohane Krisostomo, wanaodhanika kuwa watunzi wa anafora mbili zinazotumika zaidi. Iko katika Cappella Palatina, Palermo (Italia).

Liturujia ya Kimungu ni adhimisho la ekaristi kwa jina linalotumiwa hasa na Waorthodoksi na Wakatoliki wa Mashariki wanaofuata madhehebu ya Kigiriki.

Baada ya liturujia ya maandalizi, ina sehemu kuu mbili: moja ambayo inaruhusu wakatekumeni kuhudhuria, ya pili ni kwa ajili ya waamini waliobatizwa tu.

Liturujia ya maandalizi

[hariri | hariri chanzo]
Meza ya pembeni ilivyo mwishoni mwa liturujia ya maandalizi.

Inafanywa na padri na shemasi peke yao ikimaanisha maisha yaliyofichika ya Yesu kabla ya kuanza utume wake.

Wanaingia kanisani, wanaheshimu picha takatifu zilizomo na kuvaa nguo za ibada.

Kisha wanaandaa mkate na divai katika meza ya pembeni.

Hatimaye shemasi analifukizia ubani kanisa lote na kutoa kauli kwa padri ili ibada ianze.

Liturujia ya wakatekumeni

[hariri | hariri chanzo]
Padri akiingia patakatifu akishika kitabu cha Injili.
Somo la Injili.
Litania ya wakatekumeni.

Sehemu hii ya hadhara inaleta hasa Neno la Mungu kutoka Biblia ya Kikristo.

Inaanza na baraka ya padri juu ya altare kwa kutumia kitabu cha Injili.

Zinafuata litania na antifona kadhaa.

Halafu padri anaingia rasmi katika patakatifu akishika Injili.

Baada ya wimbo wa Trisagio na wa Zaburi, inatangazwa sehemu ya Nyaraka za Mitume, halafu inaimbwa Aleluya na kusomwa sehemu ya Injili.

Inaweza kufuata hotuba.

Hatimaye kuna litania nyingine kadhaa.

Ndipo wakatekumeni wanaporuhusiwa kuondoka.

Liturujia ya waamini

[hariri | hariri chanzo]
Askofu akiingia patakatifu akibeba vipaji huku shemasi mdogo akishika chetezo.
Padri akisimama kwenye meza takatifu (altare).
Waamini wakijiandaa kupokea Ushirika mtakatifu.
Ugawaji wa Ushirika mtakatifu kwa waamini.
Askofu akifanya ishara ya msalaba kwa kitabu cha Injili juu ya kitambaa cha altare kiitwacho antimension.
Padri akiruhusu waamini kuondoka kwa msalaba wa baraka.

Ndiyo adhimisho la ekaristi yenyewe kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

Baada ya litania mbili na wimbo wa Kikerubi padri anaingiza katika patakatifu vipaji vya mkate na divai kwa maandamano.

Inafuata litania nyingine, halafu busu la amani, Kanuni ya Imani ya Nisea-Konstantinopoli na anafora mojawapo, ambayo ndiyo kiini cha liturujia ya Kimungu ambamo vipaji vinageuzwa kuwa Mwili na Damu ya Kristo.

Inafuata litania nyingine tena, halafu inasaliwa Sala ya Bwana.

Kisha kuinamia Ekaristi, inatangazwa kwamba Matakatifu hayo ni kwa ajili ya watakatifu.

Wakati wa kuimba, ekaristi inaandaliwa kwa ajili ya kuliwa.

Hapo waamini wanalishwa Ushirika mtakatifu, halafu kuna nyimbo na sala mbalimbali (hata hotuba kama haijatolewa baada ya masomo) kabla ya kuruhusiwa kuondoka.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Makanisa ya Kiorthodoksi

Makanisa ya Kiorthodoksi ya Mashariki

Kanisa Katoliki la Kimelkiti

Kanisa Katoliki la Armenia

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Kimungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.