Libido

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Libido (yaani nyege au ashiki) ni uchu au hamu ya kujamiana ambayo hupatikana kwa wanaume na kwa wanawake. Neno hili la Kilatini hutumika hasa mtu alipo na kiwango kidogo cha libido. Hapo ndipo utakaposikia kwamba fulani ana libido kidogo ama mwanamume fulani amekosa nguvu za kiume. Hata hivyo, yafaa ijulikane kwamba kuna tofauti kati ya hamu ya ngono na nguvu za kiume. Mwanamume asiye na nguvu za kiume huenda akawa na kiasi cha libido kinachofaa, lakini hawezi kujamiana na mwenziwe kwa njia inayofaa maana mwili wake hauitikii.

Libido husababishwa na nini[hariri | hariri chanzo]

Libido huathiriwa na sababu tofauti kama vile za biolojia, saikolojia na za kijamii.

Libido huathirika kibiolojia kwa maana homoni za mwili, kama vile tesistosteroni na dopamini, husababisha mtu awe na uchu wa ngono au akose.

Unapokuwa na shida za kisaikolojia kama vile huzuni, wasiwasi au jambo linalokusumbua kiakili, basi uchu wako wa ngono pia utakwenda chini.

Kijamii, huenda ikawa kwamba kazi unazozifanya ili kukidhi mahitaji ya kila siku zinakunyima wakati au hata uchu wa ngono.

Libido huenda ikaathirika iwapo u mgonjwa maana hutakuwa na uchu au hata fikra za ngono.

Libido na umri[hariri | hariri chanzo]

Utafiti umeonyesha kwamba wanaume huwa na libido ya kiwango cha juu wanapobalehe kati ya umri wa miaka kumi na tano hadi kumi na tisa. Kutoka hapo, libido yao yaenda ikididimia maana homoni ya tesistosteroni pia yafifia. Hata hivyo inasemekana [1] kuna uwezekano mtu akawa na libido hafifu akiwa na umri mdogo ikiwa homoni yake ya tesistosteroni imekwenda chini, jambo ambalo linaweza kusuluhishwa .

Kwa upande mwingine, wanawake hupata libido ya kiwango cha juu zaidi wanapofikia umri wa miaka thelathini. Ijapokuwa wao huanza tamaa ya ngono wakibalehe, hamu yao huwa juu zaidi wakiwa wenye umri huo wa miaka thelathini.

Dawa za kutitimua libido[hariri | hariri chanzo]

Kwa wanaume walio na libido iliyo chini, kuna dawa ambazo waweza wakapewa na madaktari. Madawa haya, yanayotengenezwa kwa kemikali, au mata oganiki ikiwemo bidhaa zinazotolewa kwa mimea, wanyama na pia wadudu kama Spanish Fly, huwasaidia kuongezea kiwango cha homoni ya tesistosteroni testogen.

Kuna vyakula pia vinavyoongeza libido kama vile ndizi, tini na parachichi. Matunda hayo hujulikana kama mkuyati (kwa Kiingereza aphrodisiacs)[2]. Mimea mingine mikuyati ni kama vile Muyohimbi (Pausinystalia yohimbe) wa Afrika Magharibi, Mkombelo (Mondia whytei) kutoka sehemu tofauti za Afrika na Muashwagandha kutoka Uhindi (Withania somnifera).[3]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Libido kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.