Kinara cha taa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kinara cha matawi matano
Kinara cha umeme

Kinara (kwa Kiing. candelabra) ni kifaa cha kusimamishia mishumaa ndani yake ili itumike kama taa [1]. Huwa na idadi ya matawi ambayo kila moja linabeba mshumaa mmoja. Siku hizi kuna pia vinara vyenye balbu ilhali umbo la kinara huchaguliwa kama pambo la nyumba.

Katika historia kulikuwa na vinara ambavyo mafuta badala ya mishumaa yanawaka. Kinara cha aina hiyo ni menorah ya Kiyahudi yenye matawi 7.

Vinara hujulikana kutoka tamaduni mbalimbali ya kale[2].

Jina la Kiswahili limetokana na mnara likiwa na maana ya "mnara mdogo".

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Ling. Kamusi Kuu ya Kiswahili "stendi ya mshumaa unapokuwa umewashwa"
  2. 1911 Encyclopædia Britannica/Candelabrum
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.