KUSOTU

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya KUSOTU.

Katika utarakilishi , kumbukizi soma tu (kwa kifupi: KUSOTU; kwa Kiingereza: Read-only memory au ROM) ni aina ya kumbukizi (kwa usahihi zaidi, kumbukizi si-fukivu) inayotumika kwenye tarakilishi na mashine nyingine ya kielectroniki.

Data za KUSOTU haziwezi kubadilika baada ya utengenezaji wa kifaa cha kutunzia hiki. Hivyo KUSOTU inatumika kutunzia data za programu zinazobadilika kwa nadra.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Kiputiputi, O. (2011). Kamusi sanifu ya kompyuta. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, K.602.