Hekla

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hekla.
Hekla ikiwa hai kwenye ramani ya Iceland ya 1585.

Hekla ni volkeno iliyopo kusini mwa Iceland yenye kimo cha mita 1491.

Umbo la mlima ni refu: linafanana na safu yenye urefu wa kilomita 40 na kuna kasoko mbalimbali.

Hekla ni volkeno hai inayojulikana kuwa ililipuka zaidi ya mara 20 tangu mnamo mwaka 1104 BK. Kutokana na milipuko hii ya mara kwa mara imeitwa pia "geti la jahanamu".

Milipuko yake ilifunika mara kadhaa uso wa kisiwa cha Iceland, jumla ya majivu ya kivolkeno na fuwawe iliyotemwa na kasoko zake imekadiriwa ni km³ 5 na lava zake kuwa na kiasi cha km³ 8 katika kipindi cha miaka 1000 iliyopita.

Hekla pamoja na Iceland yote iko mahali ambako mabamba ya gandunia yanakutana, ambao ni bamba la Amerika ya Kaskazini na bamba la Ulaya-Asia na hapo ni sehemu ambako mara kwa mara magma ya ndani ya dunia inatoka nje.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hekla kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.