Fuwawe


Fuwawe (pia: fuwe; ing. pumice) ni aina ya mwamba mwepesi inayoundwa na povu ya zaha.
Maana yake zaha, ambayo ni mwamba joto sana katika hali ya kiowevu, inarushwa kutoka volkeno kwa shinikizo kubwa na inakuwa kama povu kwa sababu shinikizo linapungua haraka sana. Ikipoa haraka umbo hilo linaganda kuwa thabiti na kubaki vile.
Kwa hiyo asili ya fuwawe ni daima mlipuko wa volkeno.
Fuwawe inatokea kama mkusanyiko wa vipande-vipande au pia kama maganda manene.
Mara nyingi ni nyepesi kiasi kwamba inaelea juu ya maji, angalau kwa muda hadi maji yanapoingia na kujaza polepole nafasi ndani yake.
Kitamaduni inatumiwa kwa kusugua na kusafisha ngozi. Fuwawe iliyosagwa inatumiwa pia kwa kusafisha meno kwa msaada wa mswaki.
Kuna pia matumizi ya fuwawe kwa ujenzi maana ni kifaa chepesi chenye tabia nzuri za kuhami dhidi ya baridi na joto. Kwa kawaida inapondwa na kuchanganywa na kiasi kidogo cha saruji[1] lakini kuna pia majaribio ya kuitumia vile.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ When technology fails - Pumice Crete, uk. 161, via google books, ilitazamiwa Juni 2016
- ↑ Building with pumice
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- University of Oxford - image of pumice. Ilihifadhiwa 26 Julai 2020 kwenye Wayback Machine. Retrieved 2010-09-27.
- Analytical identification of a single source pumice from Greek shores and ancient sites in the Levant
- On the occurrence of a pumice-rich layer in Holocene deposits of western Peloponnesus, Ionian Sea, Greece. A geomorphological and geochemical approach.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Fuwawe kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |