Genadi wa Astorga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Genadi.

Genadi wa Astorga, O.S.B. (kwa Kihispania: Genadio, Juanacio[1]; Leon, Hispania, 865 - Peñalba de Santiago, 936) alikuwa mmonaki Mbenedikto nchini Hispania akawa abati.

Alifanywa askofu wa Astorga miaka 899 - 920 akawa mshauri wa wafalme, lakini, akitamani kurudia umonaki, alijiuzulu akaishi kama mkaapweke hadi kifo chake[2] .

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 25 Mei[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.