Edward Cummings

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Edward Cummings.

Edward Estlin Cummings (kwa kifupi E. E. Cummings; 14 Oktoba 1894 - 3 Septemba 1962) alikuwa mshairi[1] na mwandishi mashuhuri kutoka Marekani. Kwa jumla aliandika na kuchapisha mashairi, riwaya na tamthilia mia tisa. Vile vile, Cummings alijulikana sana kama mchoraji wa picha kadhaa zilizovutia.

Mashairi ya Cummings yaligusia sana masuala ya mapenzi na mazingira - alipenda sana kuandika juu ya majira ya kuchipua. Mashairi yake yalipata umaarufu kwa sababu hayakuakifishwa kama ilivyo kawaida.

Watalaamu wengi wanaamini kuwa Cummings alikuwa mmojawapo wa washairi waliojulikana sana kule Marekani katika karne ya 20. Mashairi aliyoandika Cummings, na ambayo yanajulikana sana, ni kama: "In Just Spring", "A Man Who Had Fallen Amongst Thieves", "The Cambridge Ladies" na "Buffalo Bill".

Vitabu[hariri | hariri chanzo]


Baadhi ya tuzo alizopewa[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Edward Cummings kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.