Nyoka-miti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Dipsadoboa)
Nyoka-miti
Nyoka-miti marumaru (Dipsadoboa aulica
Nyoka-miti marumaru (Dipsadoboa aulica
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Colubridae (Nyoka walio na mnasaba na kipiri)
Oppel, 1811
Nusufamilia: Colubrinae (Nyoka wanaofanana na kipiri)
Oppel, 1811
Jenasi: Dipsadoboa Günther, 1858
Ngazi za chini

Spishi 10:

Nyoka-miti ni nyoka wa jenasi Dipsadoboa katika familia Colubridae. Amepewa jina hili kwa sababu hukaa mitini takriban masaa yote.

Nyoka hawa ni warefu kiasi, m 1.4 kwa kipeo lakini sm 60-90 kwa kawaida. Rangi yao ni kijani au kahawia. Spishi kahawia zina kilingo kama marumaru. Rangi hizi zinaweza kuchukuliwa kama rangi za kamafleji.

Kama jina lao linadokeza huishi mitini ambapo hukamata vyura, mijusi-kafiri na vinyonga.

Chonge ni meno ya nyuma lakini sumu yao haina hatari kwa watu.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyoka-miti kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.