Desibeli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Desibel (kutoka Kiingereza: decibel; kifupi: dB) ni kizio cha upimaji wa nguvu au ukali. Kinalinganisha vipimo viwili kwa kutumia logi.

Matumizi yake ni hasa katika upimaji wa sauti na katika teknolojia ya umeme kwa kutaja kuongezeka au kupungua kwa volteji au sauti.

Kizio cha msingi ni "bel" na desibel ni sehemu yake ya kumi.

Nyongeza ya desibeli 3 inalingana takriban na kuzidisha nguvu mara mbili.

Kizio cha msingi cha bel kilipata jina lake kwa kumbukumbu ya Alexander Graham Bell aliyekuwa mmoja wa wabunifu wa simu.

Mara nyingi, desibeli hutumiwa kutaja ukubwa wa sauti kulingana na jinsi tunavyoisikia.

Decibel si kipimo sanifu cha SI.

Baadhi ya mifano ya sauti ni:

Kiwango cha Sauti Mifano
171 dB Karibu na bunduki kubwa ikipiga risasi
150 dB Karibu na injini ya ndege
110-140 dB Injini ya ndege kwa umbali wa mita 100
130-140 dB Watu wengi huanza kuhisi maumivu
130 dB Baragumu (umbali wa nusu mita)
120 dB Tarumpeta ya Vuvuzela (kwa umbali wa mita 1), hatari ya uharibifu wa sikio
80-90 dB Trafiki kwenye barabara kuu
60-80 dB Gari la abiria
40-60 dB Mazungumzo ya kawaida
20-30 dB Chumba tulivu sana
10 dB Jani kung'aa, kupumua kwa utulivu
0 dB Sauti ndogo kabisa inayosikika karibu na sikio

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Desibeli kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.