Clotilde Niragira

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Clotilde Niragira
Kazi yake mwanasiasa na mwanasheria wa Burundi

Clotilde Niragira (1968 - 19 Februari 2021) alikuwa mwanasiasa na mwanasheria wa Burundi. Alihudumu kama mkuu wa wizara tatu tofauti katika serikali ya Pierre Nkurunziza na alikuwa Katibu Mkuu wa Tume ya Ukweli na Maridhiano ya nchini Burundi.

Clotilde Niragira alizaliwa katika Jumuiya ya Bugenyuzi katika Mkoa wa Karuzi, mnamo mwaka 1968. Aliolewa na alikuwa na watoto watatu na alikuwa wakili kabla ya kuingia kwenye siasa.[1] Mwaka 2005 aliteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Mlinzi wa Mihuri ya Serikali katika Baraza la Mawaziri la nchi hiyo na Rais Pierre Nkurunziza. Mnamo 2006, Niragira aliidhinisha kuachiliwa kwa wafungwa 3,300.[2] Aliteuliwa kuwa Waziri wa Utumishi wa Umma, Kazi na Usalama wa Jamii, na Nkurunziza katika mabadiliko ya baraza la mawaziri tarehe 14 Novemba 2007.[3][4]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]