Bata mkia-ngumu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bata mkia-ngumu
Bata kichwa-cheupe
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Anseriformes (Ndege kama mabata)
Familia: Anatidae (Ndege walio na mnasaba na mabata)
Nusufamilia: Oxyurinae
Swainson, 1831
Ngazi za chini

Jenasi 4, spishi 10:

Mabata mkia-ngumu ni ndege wa maji wa nusufamilia Oxyurinae katika familia Anatidae. Manyoya ya mkia wao ni makavu na yametandawaa mara nyingi. Rangi ya dume ni kahawia au kahawiachekundu na domo lake lililovimba msingini ni buluu; jike ni mweusi au kijivu wenye domo la rangi ile ile. Spishi hizi huzamia kabisa ili kutafuta chakula. Hula mimea na invertebrata ya maji. Miguu yao iko nyuma sana, kama ile ya mabata wazamaji, ili kujisogeza mbele vizuri ndani ya maji. Kwa sababu hiyo hawawezi kutembea vizuri. Hujenga tago lao ndani ya uoto mzito wa maji. Jike huyataga mayai 3-8, lakini pengine hadi mayai 12 yanapatikana kwa sababu jike mwingine ameongezea mayai yake.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Spishi ya kabla ya historia[hariri | hariri chanzo]

  • Biziura delautouri (De Lautour's or New Zealand Musk Duck, Holocene ya New Zealand)
  • Tirarinetta kanunka (Piocene ya Australia Kusi)

Picha[hariri | hariri chanzo]