Armando Guebuza

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Armando Guebuza Rais wa Msumbiji.

Armando Guebuza (alizaliwa Murrupala katika jimbo la Nampula, Msumbiji, 20 Januari 1943) alikuwa rais wa Msumbiji katika miaka 2005-2015.

Katika vita vya uhuru dhidi ya Ureno alikuwa kiongozi na jenerali muhimu wa chama cha FRELIMO ambacho alijiunga nacho akiwa na umri wa miaka 20.

Kwa ufupi baada ya uhuru akawa waziri katika serikali ya Samora Machel na hatimaye rais.

Mnamo Agosti 2021, mtoto wake Ndambi Guebuza alihukumiwa kwa ufisadi.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Armando Guebuza kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.