Nachingwea
Wilaya ya Nachingwea ni wilaya moja ya Mkoa wa Lindi. Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 162,081 [1].
Wilaya hii imepakana na wilaya za Ruangwa upandw wa kaskazini Lindi Vijijini upande wa mashariki halafu na mikoa ya Mtwara na Ruvuma upande wa kusini.
Nachingwea kuna hospitali, Chuo cha Ualimu, shule za sekondari 3 na za msingi 81 wilayani.
Eneo hili lilikuwa sehemu ya mradi wa karanga wakati wa ukoloni wa Uingereza.
Kuna madini ya nikeli katika Nachingwea na kampuni ya IMX Resources NL (zamani Goldstream Mining) kutoka Australia imeanzisha kampuni "Continental Nickel" ya kuchimba nikeli hii lakini 2008 bado imetafuta pesa kwenye soko la hisa ya Kanada.
Yaliyomo |
Asili ya Nachingwea [hariri]
Neno Nachingwea asili yake imetokana na mti mmoja uliokuwa ukiitwa Ngwea. Wakazi wa makao makuu ya wilaya ya Nachingwea wakati huo Ruponda walikuwa wakienda kuchota maji chingi ya mti wa Ngwea, kwa hiyo walikuwa wakisema Nachi Ngwea wakimaanisha naenda kwenye Ngwea, yaani maana yake nakwenda kuchota maji kwenye ngwea, ndipo jina hilo Nachingwea likashika kasi na kuwa Nachingwea ya leo. Makao makuu ya mwanzo ya Nachingwea yalikuwa Ruponda.
Utawala [hariri]
Wilaya ya Nachingwea ina kata zifuatazo:
- Chiola
- Kiegei
- Kilima Rondo
- Kilimani Hewa
- Kipara Mnero
- Lionja
- Marambo
- Matekwe
- Mbondo
- Mkoka
- Mkotokuyana
- Mnero
- Mnero Ngongo
- Mpiruka
- Mtua (Nachingwea)
- Naipanga
- Naipingo
- Namapwia
- Namatula
- Nambambo
- Namikango
- Nangowe
- Nditi
- Ndomoni
- Ruponda
- Stesheni (Nachingwea)
Viungo vya Nje [hariri]
Picha za Nachingwea kwa Flikr [www.minebox.com/story.asp?articleId=8937 ]
Marejeo [hariri]
| Kata za Wilaya ya Nachingwea - Tanzania | ||
|---|---|---|
|
Nambambo | Kilimani Hewa | Ruponda | Mnero | Namapwia | Kipara Mnero | Lionja Namikango | Nditi | Kilima Rondo | Mbondo | Kiegei | Mkoka | Chiola | Mpiruka | Nangowe | Mkotokuyana | Naipanga | Stesheni | Naipingo | Mutua | Mnero Ngongo | Matekwe | Marambo | Namatula | Ndomoni |
||
| Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Nachingwea kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |