Geltrude Comensoli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha yake halisi.

Geltrude Comensoli (Bienno, Brescia, 18 Januari 1847Bergamo, 18 Februari 1903) alikuwa mwanamke wa Italia kaskazini ambaye, baada ya kushindwa na ugonjwa kujiunga na shirika la Bartolomea Capitanio, Masista wa Upendo wa Lovere wanaoitwa kwa kawaida Masista wa mtoto Maria, aliishi kibikira hadi alipofaulu kuanzisha shirika lake mwenyewe kwa ajili ya kuabudu ekaristi na kulea vijana. Jina lake la awali lilikuwa Caterina[1].

Alitangazwa mwenye heri na Papa Yohane Paulo II tarehe 1 Oktoba 1989, halafu mtakatifu na Papa Benedikto XVI tarehe 26 Aprili 2009[2][3].

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe ya kifo chake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.