Nenda kwa yaliyomo

Yohane wa Brebeuf

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Yohane alivyochorwa.
Wajesuiti wafiadini wa Amerika Kaskazini.

Yohane wa Brebeuf, S.J. (Condé-sur-Vire, Normandy, Ufaransa 25 Machi 1593 karibu na Midland, Ontario, Kanada, 16 Machi 1649) alikuwa padri wa Wajesuiti mmisionari kwa Wahuroni wa Amerika Kaskazini tangu mwaka 1625 (isipokuwa 1629 - 1633)[1].

Alikamatwa pamoja na Waindio hao, akateswa kikatili sana akauawa na Wairoki, kabila lingine la Waindio[2].

Alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenye heri tarehe 21 Juni 1925, na kuwa mtakatifu tarehe 29 Juni 1930[3].

Sikukuu ya kundi lake [4] la wafiadini huadhimishwa tarehe 19 Oktoba, lakini ya kwake mwenyewe huadhimishwa tarehe ya kifodini chake[5].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Marejeo ya Kiswahili

[hariri | hariri chanzo]
  • Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 388-390
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 363-364

Marejeo ya lugha nyingine

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.