Yohane Righi
Mandhari
Yohane Batista Righi wa Fabriano (Fabriano (Ancona), 1469 circa – Cupramontana (Ancona), 1539) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo na padri wa Kanisa Katoliki kutoka Italia.
Anaheshimiwa kama mwenye heri hasa tarehe 11 Machi.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Kisha kuzaliwa Fabriano katika familia ya kisharifu, Yohane alifuata Ukristo tangu utotoni.
Kisha kuahidi kufuata kanuni iliyoandikwa na Fransisko wa Asizi, aliishi katika konventi ya Forano.
Halafu akawa mkaapweke katika pango «La Romita», karibu na Massaccio.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Yohane Righi katika Patron Saints Index Ilihifadhiwa 4 Agosti 2011 kwenye Wayback Machine.
- 11 March saints Ilihifadhiwa 11 Februari 2008 kwenye Wayback Machine. at St. Patrick's Church