Yeriko

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Yeriko kutoka kusini.

Yeriko (kwa Kiebrania יְרִיחוֹ, kwa Kiarabu أريحا, maana yake "wenye kunukia") ni mji wa kale sana, ulioanzishwa miaka 9000 hivi KK karibu na mto Yordani.

Mwaka 2006 ulikuwa na wakazi 20,400[1][2]

Upekee wake[hariri | hariri chanzo]

Umaarufu wake unatokana na kuwa chini ya usawa wa bahari kuliko miji yote duniani.

Unasadikiwa pia kuwa mmojawapo kati ya miji ya zamani zaidi kukaliwa mfululizo hadi leo.[3][4][5]

Akiolojia imekuta chini ya ardhi zaidi ya miji 20 iliyojengwa kwa nyakati tofauti mahali pale, kuanzia miaka 11,000 iliyopita.[6]

Katika Biblia[hariri | hariri chanzo]

Katika Biblia unatajwa kama "Mji wa Mitende": chemchemi mbalimbali ndani na kandokando yake zilivuta binadamu tangu milenia nyingi.[7]

Katika Agano la Kale unatajwa kwa namna ya pekee kuhusiana na Yoshua kuingiza Waisraeli waliotoka Misri katika nchi ya Kanaani kwa kuvuka mto Yordani mkabala wa Yeriko na kuuteka kwa maandamano ya ibada (Yos 6) kabla ya miji mingine yoyote.

Katika Agano Jipya unatajwa kuhusiana na Yesu ambaye huko alimuongoa mtozaushuru tajiri Zakayo (Luk 19) na kumponya kipofu ombaomba Bartimayo (Mk 10).

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Elected City Council Municipality of Jericho Archived 5 Mei 2008 at the Wayback Machine.. Retrieved 8 Machi 2008.
  2. Projected Mid -Year Population for Jericho Governorate by Locality 2004–2006 Archived 7 Februari 2012 at the Wayback Machine. Palestinian Central Bureau of Statistics (PCBS).
  3. Gates, Charles (2003). "Near Eastern, Egyptian, and Aegean Cities", Ancient Cities: The Archaeology of Urban Life in the Ancient Near East and Egypt, Greece and Rome. Routledge. p. 18. ISBN 0415018951. Jericho, in the Jordan River Valley in Palestine, inhabited from ca. 9000 BCE to the present day, offers important evidence for the earliest permanent settlements in the Near East. 
  4. Murphy-O'Connor, 1998, p. 288.
  5. Freedman et al., 2000, p. 689–671.
  6. "Jericho", Encyclopedia Britannica
  7. Bromiley, 1995, p. 715.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: