Ungamo la Augsburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bunge la Augsburg kadiri ya Christian Beyer.

Ungamo la Augsburg ni mafundisho yaliyotungwa mwaka 1530 na wafuasi wa Martin Luther walipodaiwa kujieleza mbele ya Bunge la Dola Takatifu la Kiroma ili kurudisha umoja wa Kanisa[1].

Lengo lake lilikuwa kuendeleza matengenezo ya Kiprotestanti, lakini pia kudumisha umoja huo.

Katika sehemu ya kwanza (1-21) linafafanua mafundisho ya Kilutheri namna ya kuonyesha kwamba hayapingani na yale ya «Kanisa Katoliki au ya Kanisa la Roma».

Sehemu ya pili inazungumzia mabadiliko yaliyoanzishwa na watengenezaji ili kurekebisha mambo kadhaa yaliyotazamwa kama «maovu» (22-28), ikieleza haja ya mabadiliko hayo.

Ungamo hilo ni thibitisho tosha la nia ya Walutheri wa kwanza ya kubaki ndani ya Kanisa pekee linaloonekana.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "There is one body and one Spirit just as you were called to the one hope that belongs to your call one Lord, one faith, one baptism, one God and Father of all, who is over all and through all and in all" Ef 4:5-6
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ungamo la Augsburg kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.