Simon Patrick

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Simon Mshubirwa Patrick (alizaliwa 1 Machi 1988, katika hospitali ya Khan iliyopo mtaa wa Kisutu, wilaya ya Ilala, Jiji la Dar es Salaam) ni mwanasheria, na mwanachama wa Chama cha Mawakili Tanzania (Tanganyika Law Society) pamoja na Chama cha Mawakili cha Afrika Mashariki (East African Law Society).

Kikazi Simon ni Mkurugenzi wa Sheria na Wanachama wa klabu ya mpira wa miguu ya Young Africans Sports Club (Yanga) maarufu Young Africans S.C. nchini Tanzania. Amekuwa akitumikia cheo hiki tangu 2019. Pia amewahi kushika wadhifa wa Katibu Mkuu wa Yanga mnamo 15 Juni 2020 na Kuwa Katibu Mkuu mwenye Umri mdogo kwenye historia ya Klabu hiyo afasi aliyohudumu kwa miezi 7 baada ya Yanga kuachana na Katibu Mkuu wake wa zamani Dk. David Luhago kwa kile kilichodaiwa 'kwa maslahi mapana ya Klabu'.[1]'[2]

Novemba 17, 2020, Klabu ilimsimamisha Simon katika nyadhifa zake mara moja na kuagiza uchunguzi dhidi yake. Taarifa ilitolewa na Mshindo Msolla. Hata hivyo, tarehe 2 Juni, 2021 walimrudisha kazini na cheo chake cha zamani kama 'Mkurugenzi wa Sheria na Wanachama wa Yanga.'[3]

Katika tuhuma hizo zilizopelekea kung'olewa mbawa zake za kimamlaka, kamati huru iliyoundwa kuchunguza ilibaini kuwa si kweli kwamba alihusika katika kuhujumu kuondoka kwa Bernard Morrison Yanga. Pia si kweli kwamba alitoa faili la kisheria Yanga na hata kukutana na mmoja wa wanachama hasimu wa klabu ya Yanga Oktoba 20, 2020.[4]

Mnamo tarehe 30 Mei, 2020, Mwenyekiti wa Yanga Msindo Msolla alimfutia tuhuma zote zilizokuwa zinamkabili Simon na kuomba kuungwa mkono kwa Simon na Wanachama wa Yanga. Amekuwa akidumu katika wadhifa huo tangu hapo.

Tarehe 30 Julai 2022 Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Yanga chini ya Mhandisi Hersi Ally Said, ilimteua tena Wakili Simon kuwa Mtendaji Mkuu wa mpito kuchukua nafasi ya Bwana Senzo Mbatta Mazingiza ambaye alimaliza muda wake.

Mnano tarehe 15 Machi 2022, Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa (International Criminal Court ) ilimteua Wakili Simon kuwa Mwanasheria Msaidizi (Assistant Counsel of the International Criminal Court) wa mahakama hiyo yenye maskani yake The Hague, Netherlands barani Ulaya, na kuwa Mtanzania wa kwanza kupata nyazifa hiyo ambayo amekuwa akihudumu mpaka sasa.

Maisha na Elimu[hariri | hariri chanzo]

Simon ni wakili msomi aliyepata elimu ya uwakili katika vyuo mbalimbali nchini Tanzania. Mwaka wa 2016, alipata Stashahada ya Uzamili katika masuala ya sheria kutoka katika Chuo cha Sheria cha Dar es Salaam (The Law School of Tanzania, Dar es Salaam, Tanzania). Mwaka wa 2014, alipata Shahada ya Uzamili katika sheria za kimataifa na biashara (Master of Laws (LLM) Degree in International Law & International Trade) kutoka St. Augustine University of Tanzania.

Mwaka wa 2008-2012, alipata shahada ya kwanza ya sheria, yaani, Bachelor of Law (LLB) Degree (2008-2012) kutoka St. Augustine University of Tanzania.

Kazi na Yanga[hariri | hariri chanzo]

Kimsingi anasimamia masuala yote ya kisheria na mipango yanayohusu klabu ya Yanga. Kazi nyingine ni kupitia mikataba ya klabu ya ndani na nje ya Klabu, kutunza kumbukumbu za mikataba, kuhakikisha uhuishaji na sheria imeuatwa ipasavyo, kutoa ushauri wa kisheria, tafsiri na miongozo kwa viongozi na maafisa wakuu wa klabu kuhusu mikataba, kupitia taarifa zote na kuandaa utetezi wa kisheria kwa ajili ya matukio yoyote yale ya kisheria dhidi ya klabu na mengine mengi yanayohusu sheria.

Mbali na Klabu ya Yanga, Simon amewahi kumanya kazi mbali mbali za kisheria kwenye taasisi na makampuni mbali mbali, Amewahi kufanya kazi kama Mtafiti Msaidizi kwenye kituo cha tafiti cha chuo kikuucha Mtakatifu Agustino kilichopo Mwanza (Assistant Researcher - SAUT Center for International Law), amewahi Kuwaits mkufunzi msaidizi wa kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha Mtakatifu Agustino, Amewahi kuwa Msimamizi wa Mikataba katika kampuni ya mawasiliano Tanzania ya WiA Company Limited, baadae akapandishwa cheo na kuwa Mkuu wa Idara ya Sheria (Legal & Compliance Manager) kwenye kampuni hiyo hiyo, na bade kuwa Mkuu wa Idara ya Sheria ya Kampuni ya Mawasiliano ya Smile Telecommunications Tanzania Limited, sehemu ambayo ameanza kuhudumu tangu mwaka 2021 mpaka sasa.

Simon kwasasa anahudumu kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (International Criminal Court) kama Mwanasheria Msaidizi (Assistant Counsel of the International Criminal Court) pamoja na Mtendaji Mkuu (Chief Executive Officer) wa Klabu ya Yanga.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "YANGA SC YAACHANA NA KATIBU MKUU WAKE, DK DAVID LUHAGO WAKILI SIMON PATRICK KUKAIMU". BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE. Iliwekwa mnamo 2021-11-07. 
  2. Hasson, Felicity; Slater, Paul; Fee, Anne; McConnell, Tracey; Payne, Sheila; Finlay, Dori-Anne; McIlfatrick, Sonja (2022-06-01). "The impact of covid-19 on out-of-hours adult hospice care: an online survey". BMC Palliative Care 21 (1). ISSN 1472-684X. doi:10.1186/s12904-022-00985-6. 
  3. "Yanga suspend acting secretary-general Patrick". The Citizen (kwa Kiingereza). 2020-11-19. Iliwekwa mnamo 2021-11-07. 
  4. "YANGA SC YAACHANA NA KATIBU MKUU WAKE, DK DAVID LUHAGO WAKILI SIMON PATRICK KUKAIMU". YANGA SC YAACHANA NA KATIBU MKUU WAKE, DK DAVID LUHAGO WAKILI SIMON PATRICK KUKAIMU. Iliwekwa mnamo 2021-11-07.