Rasi ya Antaktiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Rasi ya Antaktiki kwenye bara la Antaktiki.
Ramani ya karibu ya rasi ya Antaktiki.

Rasi ya Antatiki ndio rasi kubwa kabisa huko Antaktiki. Ni sehemu ya kaskazini kabisa ya bara hilo.

Rasi ina urefu wa km 1300 kuanzia Rasi Adams kwenye Bahari ya Weddell hadi mwisho wake upande wa kaskazini uliopo kama km 1,000 kutoka Tierra del Fuego, sehemu ya kusini kabisa ya Amerika Kusini.

Kuna vituo vingi vya utafiti wa kisayansi kutoka mataifa mbalimbali pamoja na madai ya nchi hizi juu ya maeneo ya rasi.

Rasi yote inafunikwa na tabaka nene la barafu ya kudumu; hata hivyo ni sehemu ya Antaktiki ambako baridi ni nafuu kidogo. Wastani wa joto katika rasi hucheza kati ya sentigredi +1 hadi +2 kwenye mwezi wa Januari na °C −15 hadi −20 kwenye Juni. [1]

Kuna milima mingi inayofikia kimo cha mita 2,800. Kijiografia milima hiyo huhesabiwa kama sehemu ya kusini kabisa ya safu za Andes za Amerika Kusini.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.