Chapanya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pseuaspis cana)
Chapanya
Chapanya (Pseudaspis cana)
Chapanya (Pseudaspis cana)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Oda ya chini: Alethinophidia (Nyoka wasio vipofu)
Familia: Lamprophiidae (Nyoka walio na mnasaba na chata)
Fitzinger, 1843
Nusufamilia: Pseudaspidinae (Nyoka walio na mnasaba na chapanya)
Dowling & Duellman, 1978
Jenasi: Pseudaspis
Fitzinger, 1843
Spishi: P. cana
(Linnaeus, 1758)

Chapanya ni spishi ya nyoka pekee ya jenasi Pseudaspis katika familia Lamprophiidae. Anaitwa jina hili kwa sababu hula panya.

Spishi hii ni mrefu kiasi, kwa wastani m 1-1.3 lakini hadi m 1.8. Kichwa ni kidogo chenye pua fupi na bapa. Waliokomaa wana rangi moja tu: machungwa, kahawia, kijivu au nyeusi. Wachanga wana rangi zilizoiva na mabaka meusi au kahawia.

Chapanya huwinda wagugunaji katika vishimo vyao. Kinyume na jina lake hukamata mafuko hasa. Lakini wachanga hula mijusi.

Nyoka huyu hana sumu. Akitishwa anatoa sauti ya kuchata na kududia mwili na kupiga mdomo ukifunguliwa kabisa. Lakini hang'ati sana.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chapanya kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.