Nenda kwa yaliyomo

Wakarmeli Peku

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka O.C.D.)
Nembo ya shirika.

Wakarmeli Peku (kwa Kilatini Ordo Fratrum Discalceatorum B. Mariae V. de Monte Carmelo, kifupi O.C.D.) ni watawa wa Kanisa Katoliki wanaofuata urekebisho wa shirika la Wakarmeli ulioanzishwa na Teresa wa Yesu katika karne ya 16 huko Hispania. Upande wa wanaume alisaidiwa na Yohane wa Msalaba.

Mbali ya waanzilishi hao wawili, shirika lilizaa mwalimu wa Kanisa mwingine, Teresa wa Mtoto Yesu katika karne ya 19.

Kwa jumla hao watatu wanatazamwa kuwa viongozi bora kuhusu kuzama katika sala na maisha ya kiroho kwa jumla.

Pia shirika lilizaa watakatifu na wenye heri wengi.

Mwishoni mwa mwaka 2022 shirika lilikuwa na nyumba 572 zenye watawa 3,978, (kati yao mapadri 2,897).[1]

  1. Annuario Pontificio per l'anno 2022, Città del Vaticano, 2024, p. 1388

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wakarmeli Peku kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.