Nakshi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Roshani ya karne ya 18 ya mtindo wa Rococo, Bavaria, Ujerumani.
Nakshi ya Kiarabu juu ya kifaa cha Kituruki.
Sahani ya China yenye mchoro wa joka.
Kitabu cha Wendel Dietterlin, 1598.
Nakshi ya Kiislamu juu ya mlango madrasa wa Kairo, Misri.

Nakshi ni kitu chochote kinachotumika kuongeza mvuto wa uzuri wa kitu fulani.

Toka zamani za kale binadamu ameonyesha kipaji chake cha usanii kwa kutia nakshi vitu mbalimbali alivyotengeneza au alivyotumia.

Nakshi zilitumika kwa namna ya pekee upande wa dini, katika maabadi na katika vifaa vya ibada, kama vile mavazi.