Mwangati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwangati
(Terminalia spp.)
Mwangati au mpululu
Mwangati au mpululu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Myrtales (Mimea kama mkarafuu)
Familia: Combretaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mkongolo)
Jenasi: Terminalia
Spishi: T. brevipes Pamp.

T. mantaly H. Perrier
T. polycarpa Engl. & Diels
T. prunioides M.A. Lawson
T. sambesiaca Engl. & Diels
T. sericea Burch. ex. DC.
T. spinosa Engl.

Miangati ni spishi mbalimbali za mti katika jenasi Terminalia ambazo zina majani madogo kuliko mkungu (Terminalia catappa). Inatokea savana na misitu ya Afrika ya tropiki. Spishi kadhaa, k.m. T. mantaly, hupandwa katika bustani na kandokando ya mitaa. Majina mengine ni mbombaro, mkaa, mkulungo, mpululu, mwalambe, mwarambe na mwavuli. Jina mwangati hutumika pia kwa mti mwingine, Juniperus procera, unaoitwa mtarakwa vilevile.

Spishi za Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]