Mtipitipi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtipitipi
(Abrus precatorius)
Mtipitipi ukichanua
Mtipitipi ukichanua
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Planta (mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Fabales (Mimea kama mharagwe)
Familia: Fabaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mharagwe)
Nusufamilia: Faboideae
Jenasi: Abrus
Adans.
Spishi: A. precatorius
L.

Mtipitipi (pia mturituri, mchechepwa, kikwajuzi, kitimutimu, sindamu na songu; kwa lugha ya kisayansi Abrus precatorius) ni mmea mtambaa wa familia Fabaceae. Mbegu zake nyekundu na nyeusi huitwa matipitipi na hutumika kama shanga.

Matipitipi yana sumu ndani yao inayoitwa abrini na iliyo na mnasaba na risini, sumu ya mbegu za mbarika. Ganda la mbegu ni gumu sana. Kwa hivyo kumeza tipitipi lisilovunjika hakuleti shida, kwa sababu mbegu inanyewa bila badiliko. Lakini kutafuna na kumeza tipitipi moja tu kunaweza kumwua mtu mzima. Udungaji wa kiasi kidogo cha abrini unamwua mtu pia. Kwa hivyo kutoboa matipitipi na kuyatumia kama shanga ni hatari sana.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtipitipi kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.