Geita (mji)

Majiranukta: 2°52′29″S 32°13′45″E / 2.874783°S 32.229218°E / -2.874783; 32.229218
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mji wa Geita)

2°52′29″S 32°13′45″E / 2.874783°S 32.229218°E / -2.874783; 32.229218


Geita ni mji na makao makuu ya mkoa wa Geita iliyopata halmashauri yake ya pekee mnamo mwaka 2012[1].

Mji wote huwa na eneo la kilomita za mraba 1080 na maeneo yake yalitengwa na Wilaya ya Geita.

Msimbo wa posta ni 30101. [2]

Mnamo mwaka 2015 idadi ya wakazi wa Geita mjini ilikadiriwa kuwa na watu 192,541[3] Mwaka 2022 walihesabiwa 361,671 [4].

Uchumi wa Geita na kuukua kwa mji umetegemea upatikanaji wa dhahabu katika miamba ya mazingira. Uchimbaji unatekelezwa na wachimbaji wadogo na kampuni ya AngloGold Ashanti inayoajiri watu 5,000[5].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. History, Tovuti ya Geita Town Council, iliangaliwa mnamo Oktoba 2020
  2. Combined postcode list Archived 26 Julai 2018 at the Wayback Machine., mwaka 2018
  3. Makadirio ya Idadi ya Watu katika Majimbo ya Uchaguzi kwa Mwaka 2016, Tanzania Bara, Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dar es Salaam uk. 11
  4. https://www.nbs.go.tz
  5. AngloGold Ashanti, Operational profile 2019, Geita, Tanzania, taarifa ya kampuni, iliangaliwa Oktoba 2018

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Kata za Mji wa Geita - Mkoa wa Geita - Tanzania

Bombambili | Buhalahala | Bulela | Bung'wangoko | Ihanamilo | Kalangalala | Kanyala | Kasamwa | Mgusu | Mtakuja | Nyanguku | Nyankumbu | Shiloleli

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Geita bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.