Michael Faraday

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uchoraji wa Michael Faraday.
Michael Faraday katika maabara yake.

Michael Faraday (22 Septemba 179125 Agosti 1867) alikuwa mwanasayansi kutoka nchini Uingereza aliyegundua misingi muhimu kwa matumizi ya umeme. Utaalamu wake ulikuwa hasa upande wa fizikia na kemia. Aligundua mdukizo sumakuumeme akaweka hivyo msingi kwa dainamo na mashine za kutengeneza umeme. Upande wa kemia alifaulu kubadilisha gesi kadhaa kuwa kiowevu akagundua kanuni za elektrolisisi.

Ingawa Faraday hakuwa na elimu kubwa sana ya darasani na hakuwa vizuri sana katika somo la Hisabati, alikuwa ni mmoja kati ya wanasayansi maarufu sana katika Historia. Sehemu kubwa ya elimu yake Faraday alipata kwa kujisomea na kujifundisha mwenyewe. Anahesabiwa kuwa ni mwanasayansi muhimu zaidi aliyeendeleza kemia na fizikia kwa kufanya majaribio makubwa ya Kisayansi katika karne ya kumi na tisa. .[1][2]

Katika kipindi cha maisha yake, watu wengine waliokuwa kama yeye waliitwa wana falsafa asilia. Kwa kipindi hicho watu wachache tu ndio waliojulikana katika katika masuala yahusuyo umeme. Michael Faraday aligundua mambo mengi sana ikiwemo kwamba umeme unavyosafiri katika waya huwa na tabia za sumaku kwa kisasa huitwa usumaku.

Aligundua pia mambo mengi kuhusiana na namna umeme unavyoweza kutumika pamoja na kemikali ili kufanya mabadiliko katika kemikali hizo. Faraday alionesha kwamba usumaku una uhusiano wa karibu sana mwale wa mwanga.[3] Ugunduzi wake wa mota ya umeme ulitengeneza msingi wa teknolojia ya mota za umeme na kilikuwa ni kitu muhimu kutokana na juhudi zake kwamba umeme ulikuwa ni kitu rahisi kutumia katika teknolojia. Shukrani nyingi zinaelekezwa kwake kwa ugunduzi wake huo wa kwanza kwamba ni sababu ya sasa umeme umekuwa umekuwa na matumizi makubwa kwa maisha ya binadamu.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa kati ya watoto wanne wa familia maskini huko Newington Butts kusini ya London. Baba alikuwa mhunzi. Alisoma shule kwa miaka michache tu mengine akajifundisha mwenyewe. Alipofikia umri wa miaka 14 alipelekwa kama mwanafunzi kwa karahana ya kutengeneza vitabu na katika muda wa miaka saba alipata nafasi nyingi za kusoma vitabu alivyojalidi.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Russell, Colin (2000). Michael Faraday: physics and faith. New York: Oxford University Press. 
  2. "best experimentalist in the history of science" Peter Ford, University of Bath Department of Physics. Retrieved January 2007.
  3. [1] Archives Biographies: Michael Faraday, The Institution of Engineering and Technology.
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Michael Faraday kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.