Mangosuthu Buthelezi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mangosuthu Buthelezi (1983)

Inkosi Mangosuthu ("Gatsha") Ashpenaz Nathan Buthelezi (27 Agosti 1928 - 9 Septemba 2023[1]) alikuwa kiongozi wa Wazulu nchini Afrika Kusini, na vilevile kiongozi wa chama cha Inkatha Freedom Party (IFP) ambacho kiliundwa mwaka 1975.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Mangosuthu alizaliwa mnamo 27 Agosti 1928, mjini Mahlabathini, KwaZulu-Natal, na Chief Mathole Buthelezi na binti wa mfalme Magogo kaDinizulu, ambaye ni dada wa mfalme Solomon kaDinuzulu. Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Impumalanga iliyoko Mahashini, Nongoma, tangu mwaka 1933 hadi mwaka 1943, kisha katika chuo kimoja kiitwacho Adams College, kilichopo Amanzimtoti, tangu mwaka 1944 hadi 1947.

Baadaye akaelekea katika Chuo Kikuu cha Fort Hare kuanzia mwaka 1948 hadi 1950, ambapo ndipo alipojiunga na chama cha African National Congress Youth League na kuanza kupata mawasiliano na Robert Mugabe na Robert Sobukwe. Mangosuthu alifukuzwa chuoni baada ya wanafunzi kuleta mgomo. Kisha alikuja kumalizia digrii yake katika Chuo Kikuu cha Natal.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "IFP founder Mangosuthu Buthelezi has died". The Mail & Guardian (kwa en-ZA). 2023-09-09. Iliwekwa mnamo 2023-09-09. 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. William Beinart, "Twentieth Century South Africa", Oxford, 2001, pg. 330

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mangosuthu Buthelezi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.