Kitumbua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Karai la vitumbua.
Vitumbua vilivyokaangwa tayari.

Kitumbua ni aina ya chakula kinachotokana na aina ya mmea unaoitwa mpunga na hupendelewa sana na Watanzania.

Chakula hicho kinatengenezwa kwa kukaanga unga wa mchele.

Jinsi ya kukitengeneza[hariri | hariri chanzo]

  • weka mchele wako kwenye beseni lenye maji kisha uoshe vizuri
  • loweka mchele wako saa 1
  • baada ya saa moja toa maji yote uache mchele mkavu
  • twanga mchele wako uwe laini sana
  • weka maji kiasi mchele ulioutwanga weka hamira kisha koroga uwe kama uji mzito
  • weka karai jikoni tia mafuta lita 1 ya kupikia kwenye karai
  • chota uji kwa vijiko vitano kisha viweke kwenye karai lenye mafuta baada ya sekunde 60 toa weka vingine mpaka uji uishe
  • chakula chako kitakuwa tayari kwa kula.
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitumbua kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.