Khwarizmi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Muhammad ibn Mūsā al-Khwārizmī
Stempu ya Umoja wa Kisovyeti iliyotolewa kwa heshima ya sikukuu ya 1200 ya Kwarizmi
Stempu ya Umoja wa Kisovyeti iliyotolewa kwa heshima ya sikukuu ya 1200 ya Kwarizmi
Alizaliwa mnamo 780 BK
Alikufa mnamo 850
Nchi Dola la Waabasiya
Kazi yake mtaalamu wa hisabati, jiografia na falaki


Muhammad ibn Musa al-Khwarizmi (Kiarabu: محمد بن موسى الخوارزمي) alikuwa mtaalamu wa hisabati, jiografia na falaki katika dola la Waabasiya aliyeishi muda mrefu mjini Baghdad.

Alizaliwa katika familia ya Kiajemi yenye asili katika kwenye milki ya Khwarezm. Haijulikana kama yeye mwenyewe alizaliwa huko. Hakuna habari alisoma wapi.

Khwarezmi alifanya kazi kwa muda mrefu katika Dar-al-Hikma (nyumba ya hekima) iliyokuwa kama chuo kikuu kilichoundwa na khalifa Harun ar-Rashid.

Katika kitabu chake juu ya "Mahesabu kwa kutumia namba za Kihindi" alionyesha faida ya hisabati ya Kihindi akaeleza namba sifuri. Hivyo aliweka msingi wa hisabati ya kisasa. Vitabu vyake vilitafsiriwa katika lugha mbalimbali vikasambazwa kwa Kilatini pia katika Ulaya.

Ukurasa kutoka kitabu cha Khwarizmi juu ya hisabati

Aliandika pia juu ya jiografia ya Ptolemayo akashiriki katika uchoraji wa ramani ya dunia kwa matumizi ya khalifa.

Utaalamu wake kuhusu falaki alitumia kwa vitabu vyake juu ya kalenda.


Wikimedia Commons ina media kuhusu: