Kengele

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kengele ya Kaisari wa Urusi.
Petersglocke, kwenye kanisa kuu la Cologne, Ujerumani.

Kengele (kwa Kiingereza "bell") ni kifaa kilichotengenezwa kwa metali na ambacho mlio wake unafika mbali, hivyo kinatumika kujulisha ratiba fulani, kwa mfano shuleni au monasterini.

Zile kubwa zaidi zinapachikwa kwenye minara ya makanisa ili kualika waamini kusali pale walipo au kukusanyika kwa ajili ya ibada ya pamoja.

Mara nyingine zinatumika kujulisha tukio la furaha au huzuni kubwa.

Zikiwa kadhaa pamoja zinaweza kutumika pia kama ala ya muziki.

Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kengele kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.