Kanga (ndege)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanga
Kanga wa kawaida
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Galliformes (Ndege kama kuku)
Familia: Numididae (Ndege walio na mnasaba na kanga)
Jenasi: Acryllium G.R. Gray, 1840

Agelastes Bonaparte, 1850
Guttera Wagler, 1832
Numida Linnaeus, 1766

Kanga ni ndege wa familia Numididae. Jina hili ni jina la kawaida la ndege hawa, lakini spishi za Afrika ya Mashariki wana majina mengine kama chelele, chepeo, kololo, kororo na kicheleko (tazama orodha ya spishi). Kanga ni wakubwa kuliko kwale na wana rangi nyeusi na madoa meupe. Kichwa chao hakina manyoya lakini spishi tatu zina manyoya juu ya utosi. Kanga mweusi na kanga kidari-cheupe hawajulikani sana, lakini mwenendo wao unasadikiwa kufanana na ule wa spishi nyingine. Hula mbegu, wadudu, makoa na nyungunyungu, na hutaga mayai ardhini. Kanga huwa mwenzi mmoja tu maisha yao yote.

Spishi zote zinatokea Afrika. Chepeo hufugwa hususa huko Afrika ya Magharibi na pia katika Ulaya na Marekani.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: