Gerimani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Gerimani
Jina la Elementi Gerimani
Alama Ge
Namba atomia 32
Mfululizo safu Simetali
Uzani atomia 72.64
Valensi 2 na 4
Ugumu (Mohs) {{{ugumu}}}
Kiwango cha kuyeyuka 1211.40  K (938.25 °C)
Kiwango cha kuchemka 3106 K (2833 °C)
Asilimia za ganda la dunia 6 · 10-4 %
Hali maada mango

Gerimani ni elementi yenye namba atomia 32 kwenye jedwali la elementi, uzani atomia ni 72,630. Alama yake ni Ge.

Tabia[hariri | hariri chanzo]

Gerimani ni dutu mango na katika mazingira ya kawaida ni metali ngumu yenye rangi ya kifedha-nyeupe. Kiwango chake cha kuyeyuka ni 938.3 .

Ilitambuliwa mwaka 1886 na Mjerumani Clemens Winkler aliyebuni jina kwa heshima ya nchi yake ya kuzaliwa (lat. Germania)

Upatikanaji[hariri | hariri chanzo]

Hupatikana mahali pengi ndani ya madini ya shaba na zinki kwa asilimia ndogo haitokei kiasili kama elementi tupu. Huchimbwa hasa China, Urusi, Kanada, Ufini na Marekani. Uzalishaji kwenye mwaka 2011 ilikuwa mnamo tani 100. Takriban theluthi moja ya uzalishaji wake ni kwa njia ya kurejeleza.[1].

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Ilikuwa muhimu kama nusukipitishi katika vifaa vya elektroniki kama transista hadi silikoni imetumiwa zaidi badala ya Gerimani. Inatumiwa pia kwa kutengeneza vioo kwa ajili ya vifaa vya kuona nuru ya inforedi kama vile hadubini za usiku au kamera za inforedi.

  1. U.S. Geological Survey (2008). "Germanium—Statistics and Information". U.S. Geological Survey, Mineral Commodity Summaries kwa mwaka 2011