Galvanometa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Muonekano wa Galvanometa ya zamani D'Arsonval.

Galvanometa ni kifaa kilichotengenezwa kimakanika na kiumeme chenye uwezo wa kuhisi/kugundua na kupima mkondo wa umeme.

Mara nyingi Galvanometa ni kifaa cha kianalojia ambacho hutumika kama ameta kupimia mawimbi ya umeme katika sakiti ya umeme kwa kutumia kizio kiitwacho ampea.

Galvonometa hupima mkondo wa umeme kwa kutumia mshale ambao huonesha kiasi cha mkondo wa umeme kipitacho katika sakiti.

Jina linatokana na Luigi Galvani, mwanafizikia wa Italia.

Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.