Buganivilia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Buganivilia
Bougainvillea spectabilis
Bougainvillea spectabilis
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Core eudicots (Mimea kama alizeti)
Oda: Caryophyllales (Mimea kama fungu)
Familia: Nyctaginaceae (Mimea inayofanana na mkwakwara)
Jenasi: Bougainvillea
Comm. ex. Juss.

Buganivilia ni jenasi ya mimea inayotoa maua yenye asili yake katika Bara la Amerika ya Kusini kuanzia Brazili na kusonga magharibi kuelekea Peru na kusini hadi Argentina kusini (Mkoa wa Chubut). Mimea hii ina maua meupe madogo. Sehemu za mimea zenye rangi kali si maua ya kweli lakini aina ya majani maalum yanayoitwa braktea. Yanahami maua.

Waandishi tofauti wanakubali kuwa kuna kati ya spishi 4 na 18 katika jenasi hii. Mimea hii iligunduliwa nchini Brazili mnamo mwaka wa 1768 na Philibert Commerçon, msomi wa mimea kutoka nchi ya Ufaransa alipokuwa akimwandama mkuu wa Jeshi la Wanamaji la Kifaransa na mpelelezi Louis Antoine de Bougainville wakati wa safari yake ya kuizunguka dunia.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Buganivilia kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.