Kinyama-kigoga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bryozoa)
Kinyama-kigoga
Koloni ta vinyama-kigoga huko De Beldert, karibu na Tiel, Uholanzi
Koloni ta vinyama-kigoga huko De Beldert, karibu na Tiel, Uholanzi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Nusuhimaya: Eumetazoa
Faila ya juu: Lophotrochozoa
Faila: Bryozoa
Ehrenberg, 1831
Ngazi za chini

Ngeli 3, oda 4:

Vinyama-kigoga (tafsiri la jina la kisayansi) ni wanyama wadogo wa maji matamu na ya chumvi wa faila Bryozoa. Ni wanyama sahili na karibu wote huishi katika makoloni yanayoshikamanisha kwenye nyuso mbalimbali, kama vile miamba, mawe, mchanga, makombe na miani. Kwa kawaida wana urefu wa takriban mm 0.5 na wana muundo maalum wa kujilisha unaoitwa lofofori (lophophore), "taji" ya minyiri inayotumiwa kwa kujilisha kwa njia ya kuchuja. Spishi nyingi za baharini huishi katika maji ya kitropiki, lakini kadhaa hupatikana katika mifereji ya bahari na maji ya maeneo ya ncha za dunia. Vinyama-kigoga wameainishwa kama spishi za baharini (Stenolaemata), spishi za maji tamu (Phylactolaemata) na spishi za baharini na pengine maji ya chumvi kidogo (Gymnolaemata). Spishi hai 5,869 zinajulikana[1]. Spishi za jenasi moja huishi peke yao, nyingine zote huishi katika makoloni.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Bock, P.; Gordon, D.P. (August 2013). "Phylum Bryozoa Ehrenberg, 1831". Zootaxa 3703 (1): 67–74. doi:10.11646/zootaxa.3703.1.14.