Birmingham Post

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Birmingham Post
Jina la gazeti Birmingham Post
Aina ya gazeti *. Gazeti la kila wiki
Lilianzishwa 1857
Nchi Uingereza
Mwanzilishi John Frederick Feeney
Mhariri Alun Thorne
Mmiliki Trinity Mirror
Makao Makuu ya kampuni Birmingham
Nakala zinazosambazwa 12,550 (Jan-Jun 2006)[1]
Tovuti http://www.birminghampost.net

Birmingham Post ni gazeti lililoanza kuchapishwa hapo awali na John Frederick Feeney kwa jina la Daily Post katika eneo la Birmingham, Uingereza katika mwaka wa 1857. Hili lilikuwa gazeti liuzwalo sana katika eneo la West Midlands, ingawaje haikuwa na ushindani kutoka magazeti mengine katika eneo hili.

Mtindo wa kuchapisha ilibadilishwa katika mwaka wa 2008. Gazeti hili liliacha kuchapisha mwatangazo katika ukurasa wake wa kwanza katika mwaka wa 1946 likaanza kuchapisha habari muhimu tu katika ukurasa huo.

Jengo la Post and Mail katika mji wa Birmingham lilifunguliwa katika mwaka wa 1965 ili kutumikia magazeti ya Post na Evening Mail lakini Post na magazeti dada yake yalihamia jengo la Fort Dunlop, maili tatu kutoka katikati wa mji, katika mwezi Agosti 2008.

Baada ya usimamizi kubadilika mara kadhaa, gazeti hilo ni kampuni shirika katika kundi la Trinity Mirror Group. Mnamo Februari 2008, gazeti hilo lilianzisha upya tovuti yake kama birminghampost.net.

Mnamo Novemba 2009, jarida lilianza kuchapishwa[1] kila wiki badala ya kila siku.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. British News Paper Archive of Publishing,Birmingham Daily Press


Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]