Biografia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Biografia (kutoka Kiingereza Biography) ni neno la kutaja habari za kweli za maisha ya mtu.

Asili ya neno ni Kigiriki, hasa lilitaja bios (= maisha) na graphein (= andika).

Biografia kwa Kiswahili kilichozoeleka ni "Wasifu", japo kumekuwa na tabia ya kukopa maneno.

Wasifu ukiandikwa na mhusika unaitwa "tawasifu" ambayo kwa Kiingereza inaitwa autobiography.

Biografia ni sehemu ya fasihi. Kupitia maandishi mbalimbali, biografia inaweza pia kutengenezewa filamu na kadhalika.

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Biografia kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.