Bata bukini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bata bukini
Bata bukini afugwaye
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Anseriformes (Ndege kama mabata)
Familia: Anatidae (Ndege walio na mnasaba na mabata)
Nusufamilia: Anserinae (Ndege wanaofanana na mabata bukini)
Vigors, 1825
Ngazi za chini

Jenasi 3:

Goose behavior

Mabata bukini ni ndege wakubwa wa maji wa familia ya Anatidae. Wanaainishwa katika nusufamilia Anserinae pamoja na mabata-maji. Mabata bukini ni ndege wakubwa sana lakini wadogo kuliko mabata-maji. Wana domo pana pia lakini shingo yao ni fupi zaidi. Wana rangi mbalimbali kama kahawia, nyeupe na nyeusi kadiri ya spishi. Hula mimea na pengine wadudu na nyungunyungu. Wanaweza kuwa wasumbufu wakiingia mashamba. Tago lao limejengwa kwa vijiti, manyasi n.k. karibu na maji na limetandikika na manyoya mororo.

Ndege hawa huzaana kwa kanda za kaskazini kabisa za dunia au juu sana ya milima. Spishi moja tu, Cereopsis novaehollandiae, huzaa katika nusudunia ya kusini na inaainishwa pengine katika nusufamilia yake binafsi. Wakati wa majira ya baridi mabata bukini huhama kanda za moto zaidi. Bata bukini hufugwa mahali pengi pa Afrika, lakini ndege mwitu hutokea tu kwa idadi kubwa huko Maroko, Aljeria na Tunesia wakati wa majira ya baridi ya Ulaya. Ndege wanaofugwa katika Afrika kusini kwa Sahara wanatokana aghalabu na bata bukini wa Uchina. Aina kadhaa zinatoka uzalishaji mtambuka wa mabata bukini wa Ulaya na Uchina.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

  • Anser albifrons (Greater White-fronted Goose)
    • Anser a. albifrons (Eurasian White-fronted Goose)
    • Anser a. elgasi (Tule Goose)
    • Anser a. flavirostris (Greenland White-fronted Goose)
    • Anser a. frontalis (Pacific White-fronted Goose)
    • Anser a. gambeli (Gambel White-fronted Goose)
  • Anser brachyrhynchus (Pink-footed Goose)
  • Anser caerulescens (Snow Goose)
  • Anser canagicus (Emperor Goose)
  • Anser cygnoides (Swan Goose)
  • Anser erythropus (Lesser White-fronted Goose)
  • Anser fabalis (Bean Goose)
    • Anser f. fabalis (Western Bean Goose)
    • Anser f. johanseni (Johansen Bean Goose)
    • Anser f. middendorffi (Middendorf's Bean Goose)
  • Anser indicus (Bar-headed Goose)
  • Anser rossii (Ross's Goose)
  • Anser serrirostris (Tundra Bean Goose)
    • Anser s. rossicus (Russian Bean Goose)
    • Anser s. serrirostris (Siberian Bean Goose)
  • Branta bernicla Brant Goose)
    • Branta b. bernicla (Dark-bellied Brant Goose)
    • Branta b. hrota (Pale-bellied Brant Goose)
    • Branta b. nigricans (Black Brant)
  • Branta canadensis Canada Goose)
  • Branta hutchinsii (Cackling Goose) - zamani iliainishwa katika B. canadensis
  • Branta hylobadistes (Nēnē-nui au Woods-walking Goose) kabla ya historia
  • Branta leucopsis (Barnacle Goose)
  • Branta ruficollis (Red-breasted Goose)
  • Branta sandvicensis (Hawaiian Goose au Nēnē)
  • Cereopsis novaehollandiae (Cape Barren Goose) pengine inaainishwa katika familia ndogo Cereopsinae

Picha[hariri | hariri chanzo]